Karibu Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Baraza lilianzishwa kwa Sheria ya Taifa ya Usimamizi wa Mazingira Na. 19 ya mwaka 1983 kama chombo cha kuishauri serikali juu ya masuala ya utunzaji endelevu wa mazingira. Baraza lilianza kazi rasmi mwaka 1986 na baadaye kupewa nguvu ya kisheria ya kusimamia hifadhi ya mazingira nchini kwa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004.
Majukumu ya Baraza ni kutekeleza shughuli za uzingatiaji na utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira; kusimamia mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira (TAM) pamoja na ukaguzi wa mazingira; kufanya tafiti za mazingira; kujenga uelewa wa mazingira kwa umma na kusimamia na kuratibu masuala yote yanayohusu mazingira kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira na Sheria nyingine zozote zilizoandikwa.
Ofisi za Kanda
Habari za Hivi Karibuni
𝗡𝗘𝗠𝗖 𝗬𝗔𝗞𝗜𝗙𝗨𝗡𝗚𝗜𝗔 𝗞𝗜𝗪𝗔𝗡𝗗𝗔 𝗖𝗛𝗔 𝗠𝗔𝗥𝗔 𝗡𝗜𝗟𝗘-𝗣𝗪𝗔𝗡𝗜
Mar 10, 2026
NEMC YAFUTURISHA SERENA
Mar 06, 2026