Eneo la Utekelezaji wa Sheria

Majukumu na Wajibu katika Kitengo cha Utekelezaji wa Sheria (Enforcement)
i.    Kufanya ukaguzi wa mazingira, uchunguzi, na ufuatiliaji pamoja na kukusanya ushahidi;
ii.    Kukusanya sampuli na kuziwasilisha kwenye maabara iliyoidhinishwa kwa ajili ya uchunguzi;
iii.       Kurekodi na kunakili taarifa yoyote kwa njia yoyote ile kwa ajili ya kutoa kielelezo mbele ya mahakama;
iv.        Kutoa adhabu za kiutawala na kisheria kwa wale wanaokiuka taratibu;
v.    Kutoa mchango wa kitaalamu wakati wa uandaaji wa nyaraka za kisheria;
vi.        Kutoa ushahidi na kuwasilisha vielelezo mbele ya mahakama;
vii.       Kutoa mafunzo kwa wakaguzi wa mazingira walioteuliwa na kuidhinishwa;
viii.   Kushughulikia malalamiko ya mazingira kutoka kwa umma na matukio yanayoripotiwa

ix.   Kuratibu na kuchakata maombi ya vibali vya usimamizi wa taka hatarishi.