Kitengo cha Manunuzi

Kitengo hiki kinaongozwa na Meneja.

Malengo

Kutoa utaalamu juu ya usimamizi wa michakato ya manunuzi.

Majukumu

  • Kusimamia manunuzi na utoaji wa shughuli zote za Zabuni za Baraza isipokuwa uamuzi na utoaji wa mkataba.
  • Kumshauri afisa masuuli katika masuala yote yanayohusu ununuzi na uondoshaji mali.
  • Kusaidia na kutekeleza utendakazi na maamuzi ya afisa masuuli na Bodi ya Zabuni.
  • Kuratibu au kusimamia manunuzi na shughuli za ununuzi wa Baraza na kupendekeza taratibu za uondoshaji mali.
  • Kuandaa nyaraka na matangazo ya fursa za zabuni; na kusimamia michakato ya zabuni.
  • Kupitia taarifa za tathmini na majadiliano na kupendekeza utoaji wa tuzo ya mkataba kwa afisa masuuli au bodi ya zabuni.
  • Kutunza na kuhifadhi kumbukumbu za mchakato ya ununuzi na zabuni na usambazaji wa bidhaa, vifaa au mali na kusimamia uondoshaji wa mali chakavu.
  • Kufanya uhakiki wa mara kwa mara na kutoa hesabu ya mali na vifaa vya Baraza ili kubaini idadi halisi iliyopo kwenye kumbukumbu.
  • Kufuatilia mara kwa mara bidhaa, vifaa au mali za taasisi nunuzi kwa lengo la kubaini matumizi mabaya ya mali na vifaa na kupendekeza hatua stahiki za kuchukuliwa.
  • Kuandaa taarifa za mara kwa mara kuhusu bidhaa, vifaa au mali zisizotumika, zisizohitajika, zilizooisha muda wake na zilizoharibika.
  • Kusimamia uagizaji wa mahitaji ya taasisi nunuzi na viwango na idadi ya bidhaa, vifaa au mali na kutunza orodha au rejesta ya mikataba ya ununuzi iliyoingiwa.
  • Kutunza na kuhuisha kumbukumbu za bidhaa, vifaa au mali za taasisi nunuzi.
  • Kuratibu shughuli za ununuzi na uondoshaji mali ndani ya taasisi nunuzi.
  • Kutayarisha na kuwasilisha ripoti za manunuzi za mara kwa mara