Kurugenzi ya Huduma za Sheria

Malengo

Kutoa utaalamu na huduma katika masuala ya kisheria

Majukumu

  • Kutoa huduma za kisheria
  • Kutoa Ufafanuzi wa kisheria kuhusu utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira, Sura 191
  • Kutoa huduma za sekretarieti katika Mikutano ya Bodi
  • Kutoa huduma za sekretarieti katika Vikao vya Menejimenti
  • Kutoa msaada kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika mashauri dhidi ya na kwa niaba ya Baraza.
  • Kukusanya taarifa na ushahidi unaotakiwa kuhusiana na  kesi.
  • Kutoa ufafanuzi wa kisheria kwa umma kuhusu uendeshaji wa Baraza
  • Kuandaa Mikataba ya kisheria na makubaliano na kusimamia utekelezaji wa masharti katika Mikataba husika  kwa kuhakikisha masilahi ya Baraza yanalindwa.
  • Kufanya marejeo na kuanzisha taratibu za kisheria za uendeshaji wa Baraza pamoja na kupendekeza maeneo yanayohitaji kuboreshwa.
  • Kuhakikisha uhifadhi salama wa hati za kisheria
  • Kupitia ripoti mbalimbali za ukaguzi na kutoa maoni ya kisheria kuhusu masuala yanayohusu madai ya Baraza kwa ajili ya utekelezaji.
  • Kuratibu upelelezi wa kesi za jinai za mazingira kwa kushirikiana na vyombo vya uchunguzi vya Serikali
  • Kushirikiana  na Mamlaka za kisheria juu ya kesi za jinai za mazingira