Kurugenzi ya Utekelezaji na Uzingatiaji wa Mazingira (DECE)

Kurugenzi hii inaongozwa na Mkurugenzi

Malengo

Kuhamasisha ufuatiliaji na utekelezaji wa Sheria ya Mazingira

Majukumu ya Kurugenzi

  • Kuandaa miongozo ya kuhamasisha uzingatiaji wa Sheria kwa jamii na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa masharti ya vyeti na vibali vya usimamizi wa Mazingira.
  • Kuandaa miongozo kwa lengo la utekelezaji wa Sheria.
  • Kujengea uwezo wadau katika masuala ya uzingatiaji na utekelezaji wa Sheria.
  • Kuwezesha, kuratibu na kupendekeza uteuzi wa wakaguzi wa mazingira.
  • Kufanya kaguzi na ufuatiliaji wa miradi wa miradi kuhakikisha inatekeleza matakwa ya Sheria ya Mazingira na Kanuni zake.
  • Kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni zake pamoja na kutoa maelekezo kwa ukiukwaji wa matakwa ya Sheria na Kanuni zake.
  • Kutoa miongozo ya namna bora ya usimamizi na utekeketezaji wa taka hatarishi na taka za kieletroniki.
  • Kusimamia na kuendesha maabara ya mazingira ya Baraza.
  • Kushughulikia malalamiko ya kimazingira pamoja na majanga yanayotolewa taarifa kwenye Baraza.
  • Kupitia na kutoa mapendekezo kwa maombi ya vibali vya utupaji majitaka yaliyochakatwa kwenye mazingira.
  • Kuchakata maombi ya vibali vya usimamizi wa taka hatarishi na taka za kieletroniki.
  • Kushirikiana na Mamlaka Udhibiti na Mamlaka zingine katika kufanya ukaguzi, ufuatiliaji na uchunguzi katika masuala ya Mazingira.