Kurugenzi ya Tathimini ya Mazingira (DESIA)

Kurugenzi inaongozwa na Mkurugenzi

Lengo

Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu tathmini ya athari kwa Mazingira na jamii kwa miradi mipya na iliyopo ianyotekelezwa.

MAJUKUMU

  • Kuratibu mchakato wa Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Jamii (TAM) na kutoa mapendekezo kwa Waziri mwenye dhamana ya mazingira kwa maamuzi ya utoaji idhini ya utekelezaji wa mradi.
  • Kuandaa Miongozo ya kusaidia ufanyaji wa TAM na kuisambaza kwa wadau
  • Kuwajengea uwezo mamlaka za serikali za Mitaa na Wizara za Kisekta kuhusu masuala ya TAM
  • Kusajili na kusimamia utendaji wa wataalam elekezi wa mazingira
  • Kuandaa na kutunza Kanzidata ya miradi iliyosajiliwa na kupata vyeti pamoja na ya wataalam elekezi wa mazingira
  • Kuandaa mikutano ya kutoa maoni (Public Hearing) kwa miradi inayogusa maslahi ya jamii
  • Kutoa elimu kuhusu masuala ya TAM kwa wadau mbali mbali
  • Kufanya mikutano wa wawekezaji ili kujadili changamoto zao na kuweka mikakati ya kuzitatua