KANDA YA KUSINI

 

UTANGULIZI

Kanda ya Kusini ni miongoni mwa Kanda 13 zilizoundwa na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kusimamia shughuli za usimamizi wa mazingira katika mikoa mitatu ya Mtwara, Lindi na Ruvuma.

Ofisi ya Kanda ya Kusini ipo katika mkoa wa Mtwara mtaa wa Rahaleo, Barabara ya Chikongola, Jengo la Rahaleo Complex, Ghorofa ya Tatu.

NGUVU YA KANDA

Ukanda wa Kusini umejaliwa rasilimali za asili zinazohitaji ulinzi wa mazingira. Kuna utafiti wa madini ya urani, uchimbaji na usindikaji wa madini, utafiti wa mafuta na gesi, mitambo ya usindikaji na mabomba ya kusafirisha gesi, makaa ya mawe, grafiti, madini jasi na dhahabu. Pia kuna misitu na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere.

Fukwe katika Mkoa wa Lindi na kuendelea hadi Hifadhi ya Bahari ya Mtwara ambapo uchimbaji wa gesi asilia unaendelea baharini na nchi kavu, pamoja na fursa zote za Uchumi wa Buluu, zinaufanya Ukanda huu kuwa kitovu cha kitaifa na kimataifa.

Kanda ya Kusini  ni miongoni mwa kanda 13 za Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Kanda ya Kusini ilianzishwa Mwezi April , 2013 kwa lengo la kusogeza huduma za NEMC kwa wananchi wa Mikoa ya kusini Pamoja na Wilaya zake. Kanda ya Kusini inahudumia mikoa Mitatu ya  Mtwara, Lindi na Ruvuma yenye jumla ya wilaya 15 na Halmashauri 23. Shughuli kubwa katika kanda ni uchimbaji na usafirishaji wa makaa ya  mawe, utafiti, uzalishaji na utakataji wa gesi asilia, Uchimbaji na uchakataji wa madini ya Bunyu, gypsum,na Dhahabu. Aidha, Shughuli  za utafiti,  uchimbaji na uchenjuaji wa majaribio  wa madini ya  Urani zinafanyika   katika  Kanda ya Kusini hususani katika Mkoa wa  Ruvuma.    

MAJUKUMU YA KANDA

Jukumu kuu la Kanda ni utekelezaji wa uelewa wa mazingira, uratibu wa Tathmini ya Athari za Mazingira na Jamii, uzingatiaji wa sheria za mazingira na usimamizi wake ili kuendana na Dira na Dhamira ya Baraza.Maelezo ya Kina ya Kanda liliambatana na majukumu mengine kama yalivyoorodheshwa hapa chini; 

  • Kukuza weledi juu ya masuala ya Mazingira
  • Kufanya ufuatiliaji juu ya Uzingatiaji wa Sheria ya Mazingira
  • Mapitio ya Tathmini ya Athari  ya Mazingira kwa miradi ya maendeleo na uwekezaji
  • Kupokea na kutatua malalamiko ya kimazingira
  • Kupokea na kufanya mapitio ya vibali vya taka hatarishi
  • Kufanya tafiti za kimazingira

Mawasiliano

NEMC - Kanda ya Kusini,

S.L.P. 1259,

Mtwara.

Simu: +255 232334683,

Barua Pepe: nemcmtwara@nemc.or.tz

Tovuti: www.nemc.or.tz.

 

Kauli Mbiu: Mazingira yetu : Uhai Wetu, Tuyatunze, yatutunze.